MOURINHO ‘SPECIAL ONE’ KUZURU OLD TRAFFORD.
Pia amkaribisha Ferguson, Santiago Bernabeu
![]() |
Kocha wa timu ya Real Madrid Jose Mourinho |
Kocha wa Real Madrid Jose Mourinho atahudhuria mechi baina ya klabu
hasimu nchini Uingereza ambapo atashuhudia wapinzani wake katika ligi ya
mabingwa Ulaya Manchester United watakapoikaribisha Liverpool katika dimba la Old
Trafford.
Kocha huyo amesema
anapenda kuwaona wapinzani wake wakicheza LIVE badala ya kuwafuatilia kupitia
katika vituo vya Luninga.
Anasema mechi kati ya
Liverpool na Manchester United itakuwa mechi kali ya kusisimua huku akijinasibu
kwamba ataingalia mechi hiyo kama sehemu ya burudani na kazi yake.
Real Madrid itacheza na
Manchester United katika ligi ya mabingwa barani Ulaya hatua ya 16 bora
Februari 13 katika dimba la Santiago Bernabeu huku mechi ya marejeano ikipigwa
Machi 5.
WACHEZAJI 41
WAFUNGIWA MAISHA KOREA KUSINI
Wachezaji 41 wamefungiwa kutocheza soka baada ya kupatikana na hatia ya
upangaji wa matokeo katika ligi kuu nchini Korea Kusini.
Shirikisho la Kandanda ulimwenguni FIFA limethibitisha adhabu hiyo huku
likidokeza kwamba uchunguzi ulifanywa kuanzia mwaka 2011.
Serikali nchini humo imeunga mkono adhabu hiyo kutokana na kukithiri kwa
upangaji wa matokeo katika ligi ya nchi hiyo maarufu kama K-League pia katika Volleyball,Baseball na michezo mingine.
MESSI AMPIGIA SALUTI GERD MUELLER
![]() |
Lionel Messi mchezaji bora |
![]() |
Lionel Messi Akishikilia Tuzo yake |
Licha
kutwaa tuzo ya mchezaji bora wa dunia kwa mara ya nne,Lionel Messi amemvulia
kofia gwiji wa zamani wa Ujerumani na Bayern Munich kuwa alikuwa chuma cha pua
enzi za uchezaji wake.
Lionel
Messi alisema anamheshimu Mueller kwa soka lake la uhakika na historia itendelea
kumkumbuka hivyo.
Messi
(25) raia wa Argentina alivunja rekodi ya Mueller ya kufunga magoli 85 mwaka
1972 lakini yeye amefunga magoli SITA zaidi mwaka 2012 pekee kwa kufunga magoli
91.
PSG YAMKANA
CRISTIANO RONALDO
![]() |
Christiano Ronaldo |
Mkurugenzi wa mabingwa watetezi wa
kombe la ligi kuu nchini Ufaransa klabu ya Paris Saint-Germain Leonardo amekanusha
uvumi ulioenea kuwa mshambuliaji wa klabu ya Real Madrid
CRISTIANO DOS SANTOS RONALDO yuko mbioni kujiunga na klabu hiyo
inayoshiriki ligi kuu nchini ufaransa.
Hata kocha Carlo Ancelotti wa PSG
amekanusha uvumi huo.
Ikumbukwe
kuwa mshambuliaji huyo kutoka nchini ureno mwanzoni mwa msimu huu alisema kuwa
anafuraha kuendelea kuichezea klabu ya Real Madrid baada ya kuongezwa kwa ushuru nchini
uhispania.
Lakini naye kiungo wa klabu ya Swansea Pablo
Hernandez amesema anaamini kuwa mashabiki wa klabu ya Chelsea the blues watampa
mda wa kutosha kocha wa klabu hiyo Mhispania RAPHAEL BENITEZ ili klabu hiyo
iweze kutulia.
0 comments:
Post a Comment