Naibu Mkurugenzi wa Mawasiliano Tanzania (TCRA) Bwana Victor Nkya

Imeeelezwa kwamba gharama za mwingiliano  mawasiliano ya simu kutoka mtandao mmoja  kwenda mtandao mwingine zinatakiwa  kupitiwa  upya ili kumpunguzia mzigo kwa wananchi.

Akiongea wakati  wa mjadala kuhusiana na gharama hizo Naibu Mkurugenzi  wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania TCRA Victor Nkya amesema utafiti unaonesha kuwa gharama zinaweza kupunguzwa zaidi na kuwanufaisha watumiaji wa simu za mikononi.

Bwana Nkya amesema baada ya utafiti TCRA imeona kwamba mwananchi aweza kutumia shilingi 34.9 badala ya shilingi 113  ambazo zinatumika katika mitandao ya simu kwa hivi sasa.

Hata hivyo kwa upande wa wadau hususani wawakilishi  wa kampuni zinazotoa huduma za simu wameonekana kutofautiana kimsimamo kwani wengi wanaonekana kutounga mkono wazo la kushusha gharama kuanzia mwezi Machi mwaka huu.

Wawakilishi hao wamesema hofu yao kubwa ni kushindwa kumudu   gharama kubwa za uendeshaji hivyo huenda wakajiendesha kwa hasara na hatimaye kufilisika.

Kwa upande wa wananchi wamesema kama pendekezo hilo litapitishwa litawapa ahueni kwani wamekuwa wakiingia gharama kubwa wanapowasiliana kutoka Mtandao mmoja hadi mwingine.
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

0 comments:

 
Top