Pambalo
la watani wa jadi Simba na Yanga la Ligi Kuu ya Vodacom lililochezwa jana (Mei
18 mwaka huu) kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam na kumalizika kwa mabingwa
wapya Yanga kushinda mabao 2-0 limeingiza sh. 500,390,000.
Mechi
hiyo namba 180 ambayo ilikuwa kati ya saba la kuhitimisha ligi hiyo msimu wa
2012/2013 ilishuhudiwa na watazamaji 57,406 waliokata tiketi kwa viingilio vya
sh. 5,000, sh. 7,000, sh. 10,000, sh. 15,000, sh. 20,000 na sh. 30,000.
Kila
klabu imepata mgawo wa sh. 123,970,927.45 wakati Kodi ya Ongezeko la Thamani
(VAT) iliyolipwa ni sh. 76,330,677.97.
Kiingilio
cha sh. 5,000 ndicho kilichovutia watazamaji wengi ambapo waliokata tiketi hizo
walikuwa 19,039 na kuingiza sh. 95,195,000 wakati kile cha sh. 7,000 kiliingiza
watazamaji 17,647 na kupatikana sh. 123,515,000.
Mgawo
mwingine wa mapato hayo ni asilimia 15 ya uwanja sh. 63,036,064.81, tiketi sh.
3,818,890, gharama za mechi sh. 37,821,638.88, Kamati ya Ligi sh.
37,821,638.88, Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) sh. 18,910,819.44 na
Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) sh. 14,708,415.12.
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI
0 comments:
Post a Comment