Serikali ya Tanzania na China zimeandaa mdahalo ambao utahusisha nchi mbalimbali ukiwa na lengo la kujadili fursa za ushirikiano kati ya nchi hizi mbili ambapo fursa ya  ndoto ya china katika kuleta maendeleo Tanzania na kuimarisha uhusiano kati ya China na Tanzania katika hali ambayo kila upande utanufaika.  

Mshauri wa masuala ya kisiasa wa Balozi ya China Nchini Tanzania Bwana Li Su Hang amesema ni fursa nzuri kwao kueleza mawazo yao katika ndoto yao katika Afrika kimaendeleo.

Na kaimu naibu mkuu wa chuo kikuu cha Dar Es Salaam Profesa Bonivecha Rutinwa ameeleza malengo manne ya mdahalo  huo ambayo ni fursa ya ndoto ya China  katika kutimiza malengo yao kwa Tanzania, muelekeo wa pamoja kati ya Afrika na China katika kutimiza malengo yao, fursa na changamoto katika ushirikano kati ya China na Tanzania katika mustakabali mpya na jinsi ya kuimarisha uhusiano katia ya China na Tanzania katika hali ambayo kila upande utanufaika.
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

0 comments:

 
Top