Na Magreth Kinabo, Maelezo
INAKADIRIWA kuwa asilimia saba ya idadi ya watu
wazima wanaugua ugonjwa wa kisukari, lakini chini ya 1/3 ndio
wanaofahamu wana tatizo hilo. Kauli hiyo imetolewa leo na Waziri wa Afya
na Ustawi wa Jamii, Dk. Hussein Mwinyi wakati akizindua kliniki ya
vikoba ya wagonjwa wa kisukari uliofanyika kwenye viwanja vya Mnazi
mmoja jijini Dar es Salaam.
Dk. Mwinyi alisema watu wanaokabiliwa na tatizo hilo, wanafika
hospitalini wakiwa wameathirika figo, macho, shinikizo la damu au
kukatwa miguu.
“Ninaishauri jamii kutumia huduma hiyo ili kuweza kuchunguza afya zao
na kujinga kwa kufuata kanuni za afya kama vile kula vyakula visivyo na
mafuta mengi, sukari nyingi, chumvi kiasi, kula mboga za majani kwa
wingi na matunda,” alisisitiza. Dk. Mwinyi.
Aliongeza pia jamii inatakiwa kufanya mazoezi ya kutosha, kupunguza
uzito kwa kiwango kinachotakiwa, kutovuta sigara na kupunguza kunywa
pombe au kuacha kabisa. Dk. Mwinyi alisema 1/3 ya idadi ya watu wazima
wanakabiliwa na shinikizo la damu, lakini chini ya asilimia 10 ndio
wanafahamu kuwa wameathirika na tatizo hilo.
Kwa upande wake, Katibu Mkuu wa Chama cha Wagonjwa wa Kisukari
Tanzania, Dk. Kaushik Ramaiya alisema kliniki hiyo imezinduliwa kwa
ushirikiano wa chama hicho na wizara hiyo ili kuboresha huduma za afya
nchini. Pia imetolewa na Novo Nordisk wakishikikiana na Chama cha
Wagonjwa wa Kisukari Duniani.
Alisema kliniki hiyo ambayo itakuwa na inatoa tiba kwa wagonjwa wa
kisukari hususan watoto inafaa vifaa vya kisasa kwa ajili ya upimaji wa
matatizo ya kisukari, macho, meno na mahabara ikiwemo genereta
itakatotumika sehemu ambazo hazina umeme. Pia itatoa huduma hiyo kwa
watu wazima.
Aliongeza kuwa kliniki hiyo ni ya kwanza kuzinduliwa ni maalum kwa
kanda ya ziwa ili kusogeza huduma za afya kwa wananchi. Hivyo hapo
baadae watatoa nyingine kwa ajili ya kanda zingine. Katika uzinduzi huo
jumla ya watu wapatao 79 walijitokeza kupima afya zao na kupata ushauri
mbalimbali.
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI
0 comments:
Post a Comment