MATUKIO KATIKA PICHA
Katibu
mkuu wa shirikisho la mpira wa miguu Tanzania TFF Angetile Osia
(kushoto),Kocha mkuu wa Taifa Stars Kim Poulsen na Leodgar Tenga
wakifuatilia kwa makini sherehe za makabidhiano ya basi maalum la Taifa
Stars lililotolewa na kampuni ya bia ya TBL ambao huidhamini kupitia bia
ya Kilimanjaro.
Mkurugenzi mkuu wa kampuni ya TBL Robin na baadhi ya watendaji wa kampuni
Baadhi ya wasanii wa kundi la Wanne Star wakitumbuiza wakati ya hafla hiyo.
Hili ndilo basi la timu ya taifa ya Tanzania Taifa Stars ambalo
limetolewa na kampuni ya TBL ambao ni wadhamini wa timu hiyo. Baadhi ya
sifa za basi hilo aina ya YOUTONG ni pamoja na kuwa na TV mbili
kubwa,Friji mbili sehemu ya kuwekea vifaa vya michezo,music system yenye
spika nane na tanki la kuweka mafuta lita 800,Kiyoyozi na viti 50 kwa
ajili ya abiria (wachezaji).
Katibu
mkuu wa TFF Angetile Osiah kulia akifuatiwa na Kocha Kim Poulsen,Rais
wa TFF Leodgar Tenga, mkurugenzi mkuu wa TBL Robin Goetzche na watendaji
wengine wa TBL wakishikilia mfano wa ufunguo wa basi la Taifa Stars kama
ishara ya makabidhiano rasmi ya basi hilo tayari kwa kutumika.
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI
0 comments:
Post a Comment