|
HILI NDILO LORI WALIMOPANDA VIBARUA HAO WA SHAMBA LA KAPUNGA |
|
MTOTO ALIYEJERUHIWA AKIHAMISHWA KUTOKA KATIKA HOSPITALI YA MISHENI CHIMALA NA KUPELEKWA HOSPITALI YA RUFAA MBEYA |
|
MAJERUHI AKISUBIRI KUPATA MATIBABU |
|
HAWA NI MAJERUHI |
|
KWELI MUNGU NI MKUU HUWALINDA WATOTO WADOGO HAPA MKUU WA MKOA AKIMPA POLE MOJA YA WATOTO WALIOPATA AJALI |
|
MKUU WA MKOA MBEYA ABAS KANDORO AKIONGEA NA WAANDISHI WA HABARI |
|
HILI NI ENEO LA TUKIO |
|
HAWA WOTE NI WANAFUNZI WALIOKUWA WANAENDA KUFANYA KIBARUA CHA KULIMA KWA MWEKEZAJI KATIKA SHAMBA HILO LA KAPUNGA |
|
MMOJA KATI YA MAJERUHI |
|
MAJERUHI 22 WAKIPAKIZWA KATIKA ROLI AINA YA FUSO TAYARI KUPELEKWA KATIKA HOSPITALI YA RUFAA MBEYA |
|
MAJERUHI WAKIWA KATIKA GARI AINA YA FUSO TAYARI KUSAFIRISHWA HADI HOSPITALI YA RUFAA MBEYA |
|
MAJERUHI WAKISAFIRISHWA KWENDA MBEYA |
WATU watano wamepoteza maisha na
wengine 130 wamejuruhiwa vibaya huku hali zao zikiwa mbaya baada ya Lori
walilokuwa wakisafiria shambani kuacha njia na kupinduka katika kijiji cha
Mapogolo kata ya Itamboleo Wilayani Mbarali Mkoani hapa.
Ajali hiyo imetokea leo saa 1:30
asubuhi ambapo lori hilo ambalo ni mali ya Mwekezaji wa shamba la Kapunga
Rice Project, na kwamba watu hao walikuwa wakielekea kwenye shamba la mwekezaji
huyo lililkuwa limebeba vibarua hao zaidi ya 200 ambao ni wakazi kitongoji cha
Kapunga.
"
Lori
hilo
lenye namba za usajili T398 BSE aina ya Scania Tipa, ambalo lilikuwa
likiendeshwa na
dereva aliyejulikana kwa jina Baraka Moreli, lilionekana likiwa katika
mwendo kasi na dereva huyo akiwa na lengo la kutaka kuipita
pikipiki iliyokuwa mbele yake. Huku akishangiliwa na vibarua hao ipite
ipite hiyo pikipiki haiwezi kutushinda sisi gari kubwa" moja ya majeruhi
alisema. Aliendelea kusema dipo walipofika kwenye kona dereva gari lilimshinda hilo lilimshinda na
kupinduka
Aidha, Kandoro alisema kuwa idadi
ya majeruhi katika ajali hiyo ni 130 ambapo wanawake ni 40 na
wanaume 89 huku idadi ya watoto waliokuwa wameongozana na wazazi wao haikuweza
kufahamika kwa haraka.
Akiwa Hospitalini hapo Mkuu wa
Mkoa wa Mbeya, Abbas Kandoro ambaye aliweza kufika hospitalini hapo alisema
kuwa mara baada ya kupata taarifa ya ajali hiyo kutoka kwa Mkuu wa Wilaya ya Mbarali Gullam Hussein Kiffuu, huku akiombwa kupatiwa msaada wa kuongezewa
madaktari, vifaa vya mataibu sambamba na uwezekano wa kupata damu
kwa ajili ya kuwaongezea majeruhi hao alifanikiwa kuwasiliana na uongozi wa
hospitali ya Rufaa ya Mbeya na hospitali ya Mkoa ili kuweza kuona namna ya kwenda
kuokoa maisha ya majeruhi hao.
Kandoro, alisema kuwa
katika ajali hiyo watu watano wamefariki, wanne wa kiume na mmoja ni mwanamke.Watatu wametambuliwa. Aliwataja waliotambuliwa kuwa ni Samweli Mapugilo Mbena (30) mkazi wa Ilembula, Bon Mfupa (27) mkazi wa mapogolo na Edgar Mwakipesile (35) mkazi wa Nonde, Mbeya
VIA
MBEYA YETU
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI
0 comments:
Post a Comment