Mratibu wa sherehe za mwaka mpya kwa Wachina waishio Tanzania,mwalimu
AO MAN YU (katikati) akiongea na waandishi wa habari kuhusiana na maadhimisho
ya mwaka mpya yatakayofanyika jijini Dar es Salaam mapema mwezi ujao.
Baadhi ya waratibu wa tamasha la mwaka mpya wa
Wachina waishio Tanzania wakiongea na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam
kuhusiana na maadhimisho yatakayofanyika Februari 2 – 3 mwaka huu.
Baadhi ya viongozi wa chama cha wahandisi washauri
Tanzania wakiongea na waandishi wa habari katika ukumbi wa Habari Maelezo
jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa chama cha Wahandisi washauri Tanzania
Injinia Menye Manga (katikati) akiongea na waandishi wa habari kuhusiana na
mkutano wa kimataifa wa wahandisi utakaofanyika jijini Dar es Salaam kuanzia
leo
Raia wa China wanaoishi Tanzania wanataraji kusherehekea mwaka
mpya Februari 2-3 mwaka huu kwa kushiriki katika shughuli mbalimbali
zinazoutambulisha utamaduni wa China.
Mratibu wa shughuli hizo mwalimu wa Kiswahili wa Chuo cha
Mawasiliano huko CHINA,AO MAN YU amesema kwa miaka mitatu iliyopita wamekuwa
wakiadhimisha sherehe hizo hivyo kwa mwaka huu utakuwa wa NNE tangu waanze
kufanya hivyo hapa nchini.
Mratibu huyo amechukua fursa hiyo kuwakaribisha watanzania
kushiriki katika shughuli hiyo muhimu ambayo itaambatana na michezo ya asili ya
China kama vile kungfu,karate Muziki wa asili ya china na burudani nyingine.
Mwakilishi huyo wa
China amesema Watanzania wamekuwa WABIA
wakubwa katika shughuli mbalimbali za kimaendeleo zikiwemo,utamaduni na
biashara.
Kwa mujibu wa ratiba iliyotolewa inaonesha kwamba Februari 2
shughuli za kimichezo zitafanyika katika viwanja vilivyo jirani na hoteli ya
Golden Tulip kuanzia saa 10.00 - 12.00
jioni.Siku itakayofuata kutakuwa na tamasha katika viwanja vya Mnazi Mmoja
kuanzia saa 12:00 – 20:00.
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI
0 comments:
Post a Comment