Kaimu mwenyekiti wa kamati ya bunge ya hesabu ya mashirika ya umma
(POAC) Muhammed Amour Chombo akiongea na waandishi wa habari mara baada
ya kupokea ripoti ya shirika la utafiti na maendeleo ya viwanda
Tanzania TIRDO,
Profesa Idrisa Mushoro mwenyekiti wa bodi ya TIRDO wakati wa
uwasilishaji wa ripoti ya shirika hilo mbele ya Kamati ya Bunge ya Hesabu ya Mashirika ya Umma (POAC).
Kamati ya bunge ya
hesabu za mashirika ya umma imekataa ripoti ya fedha iliyotolewa na
shirika la maendeleo ya viwanda Tanzania TIRDO kwa makosa ya kimahesabu.
Kaimu Mwenyekiti wa kamati hiyo Muhammad Chombo
amesema dosari iliyojitokeza katika
bajeti ya shirika hilo ni milioni
60 ambazo hazijulikani ziliko huku zimetumika milioni 155 kati ya milioni 216.
Kaimu Mwenyekiti huyo amesema kukosekana kwa fedha
hizo kwenye akaunti na kwenye maelezo ya ripoti ya TIRDO kunaashiria kuwepo kwa
ubadhirifu hivyo kuitaka ofisi ya mkaguzi wa hesabu za serikali CAG
kulichunguza shirika hilo.
Kamati hiyo imetoa onyo kwa kaimu Mkurugenzi wa
shirika hilo Ludovick Manege kutopindisha ukweli wa maelezo ya ripoti
vinginevyo itaonekana kuwa yuko nyuma ya madudu yote yanayofanyika katika
shirika hilo.
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI
0 comments:
Post a Comment