Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimkabidhi Naibu Waziri wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii Dkt. Seif Rashid kitabu cha kampeni ya Lishe Tanzania baada ya kukizindua leo Machi 16, 2013  katika bustani ya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam. Kulia ni Rais Mstaafu Alhaj Ali Hassan Mwinyi na kushoto ni Mama Salma Kikwete akifuatiwa na Mama Maria Nyerere

 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akizindua   kitabu cha kampeni ya Lishe Tanzania baada ya kukizindua leo Machi 16, 2013 katika bustani ya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam. Kulia ni Rais Mstaafu Alhaj Ali Hassan Mwinyi na Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Mhe Peniel Lyimo akifuatiwa na Mkurugenzi wa kwanza wa Taasisi  ya  Chakula na Lishe Mzee Lema. Kushoto ni Mama Salma Kikwete akifuatiwa na Mama Maria Nyerere

 Mama Maria Nyerere akifurahia tuzo maalumu aliyopokea kwa niaba ya Baba wa Taifa aliyotunukiwa na Taasisi ya Chakula na Lishe kwa mchango wake mkubwa kwa kukuza na kuendeleza sera ya lishe nchini wakati wa sherehe za uzinduzi wa Kampeni ya Lishe Tanzania leo Machi 16, 2013 katika bustani ya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimkabidhi Rais Mstaafu Alhaj Ali Hassan Mwinyi tuzo maalum iliyotolewa na Taasisi ya Chakula na Lishe kutambua mchango wake mkubwa katika kusimamia lishe na maendeleo yake  nchini  katika uzinduzi wa kampeni ya lishe nchini  leo Machi 16, 2013  katika bustani ya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam. Kulia ni Rais Mstaafu Alhaj Ali Hassan Mwinyi na kushoto ni Mama Salma Kikwete akifuatiwa na Mama Maria Nyerere
 
PICHA NA IKULU

TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

0 comments:

 
Top