Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,akifungua pazia kama ishara ya uzinduzi wa Tawi la Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere,huko Bububu Zanzibar leo asubuhi ,(kushoto) Mwenyekiti wa Bodi ya Chuo Dk.Salim Ahmed Salim. IMG_0773 
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,akipata maelezo kutoka kwa Mshauri wa Kitaalamu wa Chuo cha Ardhi serikali ya Muungano Dk.Staulans Ntiyakunze,(wa tatu kulia) baada ya kuzindua rasmi  Tawi la Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere,huko Bububu Zanzibar leo asubuhi ,(kushoto) Mwenyekiti wa Bodi ya Chuo Dk.Salim Ahmed Salim. IMG_0803 
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,akiangalia meza na vikalio vyake wakati alipotembelea moja ya madarasa katika  Tawi la Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere,huko Bububu Zanzibar leo, baada ya kuzindua Chuo hicho,(kushoto) Mkuu wa Chuo Dk. John Magoti, na pili kulia makamo wa kwanza wa Rauis wa Maalim Seif Sharif,akifuatiwa na Mwenyekiti wa Bodi ya Chuo Dk.Salim Ahmed Salim. IMG_0857 
Mwalimu wa Darasa la Kompyuta Julius Maungo,akitoa maelezo kwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,alipotembelea katika darasa la kompyuta leo baada ya kuzindua rasmi Tawi la Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere,huko Bububu Zanzibar leo asubuhi ,[Picha na Ramadhan Othman,Ikulu.] IMG_0866 
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,akipata maelezo kutoka kwa Mkuu wa Chuo Dk. John Magoti, baada ya kuzindua rasmi  Tawi la Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere,huko Bububu Zanzibar leo asubuhi alipotembelea sehemu mbali mbali za Chuo hicho. IMG_0875 
Baadhi ya wanafunzi wa Chu cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere Tawi la Zanzibar wakiwa katika hafla ya uzinduzi wa chuo hicho leo uliofanywa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein. IMG_0901 
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein, akipokea zawadi kutooka kwa Mwenyekiti wa Bodi ya Chuo cha Mwalimu Nyerere  Dk.Salim Ahmed Salim,wakati wa uzinduzi wa Tawi la Chuo hicho uliofanyika leo huko Bububu Nje ya Mji wa Zanzibar,
[Picha na Ramadhan Othman, Ikulu.]

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohmed Shein amevitaka vyuo nchini kutolegeza vigenzo vya udahili wa wananfunzi wanaojiunga na vyuo hivyo kwani kufanya hivyo kunaweza kuathiri ubora wa elimu na taaluma inayotolewa.
 
Dk. Shein amesema hayo leo katika hafla ya uzinduzi wa Tawi la Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere lilopoto Bububu nje kidogo ya mji wa Zanzibar.
 
“Tusilegeze masharti au vigezo vya wananfunzi kujiunga na vyuo kwa sababu kufanya hivyo kunaweza kuathiri ubora wa taaluma inayotolewa na kusababisha heshma ya chuo kushuka” alieleza
 
Alifafanua kuwa pamoja na kuwepo na vyuo vingi nchini hivi lakini wanafunzi wengi wanakimbilia katika vyuo vinavyotambuliwa kwa kutoa elimu bora na wataalamu wenye uwezo katika taaluma zao na wanaoweza kushindana katika soko la ajira.
 
“Uzuri wa taasisi ya elimu haupimwi kwa kuangalia ubora wa mazingira yanayotolewa elimu pekee bali hupimwa kwa uwezo wa taaluma wanayokuwa nayo wahitimu wake hivyo taasisi ya Mwalimu Nyerere lazima izingaite ubora wa maarifa ya wahitimu wake”alisisitiza.
 
Kwa hivyo aliitaka Menejimenti na Bodi ya chuo hicho iliyo chini ya uenyekiti wa Dk. Salim Ahmed Salim kuhakikisha kuwa elimu inayotolewa katika chuo hicho inalingana sio tu na historia ya chuo bali hadhi ya jina la Mwalimu Nyerere.
 
Rais wa Zanzibar ameipongeza Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kugharimia ujenzi wa chuo hicho ambao umegharimu zaidi ya shilingi ya bilioni 6.
 
Alisema fedha hizo zimewezesha kutekeleza Sheria Namba 6 ya mwaka 2005 ya kuanzisha Taasisi hiyo ambayo iliekeleza Taasisi hiyo iliyo na makao Mkauu yake Tanzania Bara kuwa na Tawi lake Zanzibar.
 
“Sheria hiyo(Namba 6) inatamkia wazi kwamba chuo kitakuwa na Tawi Zanzibar. Kwa kuwa Sheria ni jambo moja na utekelezaji Sheria inayohusika ni jambo jingine, napenda kuipongeza Bodi ya Chuo kwa kusimamia vyema utekelezaji wa Sheria iliyoanzisha chuo” alieleza.
 
Kwa upande wake Dk. Shein alieleza kuwa Serikali ya Mpinduzi ya Zanzibar itajitihadi kila inapowezekana kuziunga mkono jitihada za Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika kuendeleza ujenzi wa Tawi hilo la chuo.
 
“Katika kutoa mchango wake Serikali itaendelea kutoa kila aina ya ushirikiano ili kuhakikisha kuwa changamoto zinazokikabili chuo hiki zinapatiwa ufumbuzi hatua kwa hatua”alibainisha.
 
Amewataka vijana kuitumia fursa ya kuwepo kwa chuo hicho kujiendeleza kitaalamu badala ya kuendekeza mambo yasiyohusiana na masomo yao kama masuala ya siasa na migogoro ya dini pamoja na kuiga tamaduni za nje.
 
“Kwa bahati baadhi ya vijana wanapojiunga na vyuo hasa vya elimu ya juu hujisahahau na kuiga mambo yasiyolingana na utamaduni wetu,silka zetu na yaliyo kinyume na maadili yetu” alisema hivyo sivyo na kuongeza kuwa wanaofanya hivyo wanajiharibia maisha yao.
 
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Bodi ya Chuo Dk. Salim Ahmed Salim aliieleza jumuiya ya wananchuo na wageni waliohudhuria hafla hiyo kuwa Taasisi yake imefurahishwa na jinsi Serikali ya Mapinduzi Zanzibar inavyoithamini Taasisi yake.
 
Hivyo ametoa wito kwa vijana kote nchini na husan wa Zanzibar kuitumia fursa hiyo kupata taaluma mbalimbali zinakazolisaidia taifa kupiga hatua kimaendeleo.
“Mkiitumia fursa hii vyema wakati huu wa utandawazi mtakuwa mmejifanyia mema nyinyi wenyewe na taifa lakini msipoitumia vizuri tutakula hasara kubwa”alisisitiza.
 
Nae Mkuu wa Chuo hicho Dk. John Magoti aliishukuru Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kwa kuipatia hekta 81.8 ya ardhi kwa ajili ya ujenzi wa chuo hicho.
 
Akisoma taarifa ya ujenzi na majukumu ya chuo Dk. Magoti alieleza kuwa mpango wa Taasisi ni kuongeza majengo mengine mawili ili kukidhi mahitaji halisi ya nafasi kwa shughuli za utawala pamoja na masomo.
 
Alitaja changamoto zinazoikabili taasisi hiyo kuwa ni pamoja na ufinyu wa bajeti,ukosefu wa hosteli kwa wanafunzi, idadi ndogo ya udahili na vijana wa Zanzibar kutochangamkia nafasi za ajira wakati Taasisi hiyo inapotangaza nafasi hizo hivyo kusababisha wakufunzi wengi kuwa wametoka Tanzania Bara.
Rajab Mkasaba, Ikulu Zanzibar.
Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax: 024 2231822 

TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

0 comments:

 
Top