clip_image001 
Licha ya kuongezwa kwa ulinzi, bado matukio ya mauaji yameendelea kushamiri mashuleni.

Wanafunzi 29 na mwalimu mmoja wameuawa baada ya Waislamu wenye msimamo mkali kuvamia shule ya bweni kaskazini mashariki mwa Nigeria.
 
Walionusurika, ambao wamekuwa wakitibiwa majeraha ya moto na risasi, wamesema baadhi ya wanafunzi walichomwa moto wakiwa hai katika shambulio hilo jana kwenye Shule ya Sekondari ya Serikali mjini Mamudo katika jimbo la Yobe.
 
Mkulima Malam Abdullahi alilia juu ya miili ya watoto wake wawili wa kiume, wenye umri wa miaka 10 na 12.
 
"Hivyo ndivyo ilivyo, ninawahamisha watoto wangu wengine wa kiume kutoka kwenye shule hii," alieleza Malam. Alisema alikuwa na watoto wengine wadogo watatu kwenye shule moja ya jirani na hapo.
 
Alisema hakukuwa na ulinzi kwa wanafunzi licha ya kuwapo maelfu ya wanajeshi tangu serikali ilipotangaza hali ya hatari katikati ya Mei kwenye majimbo matatu ya kaskazini-mashariki.
 
"Tulikuwa tumelala ndipo tukasikia milio ya risasi.Nilipoamka, mtu mmoja alikuwa kanielekezea mtutu wa bunduki," alisema Musa Hassan mwenye umri wa miaka 15.
 
Aliinua mikono yake juu kujilinda, na kujeruhiwa kwa risasi zilizolipua vidole vyake vyote vinne kwenye mkono wake wa kulia, vile anavyovitumia wakati wa kuandika.
 
Alisema watu hao wenye bunduki walikuja na mapipa yaliyojaa mafuta ambayo walitumia kuchoma moto jengo la utawala la shule hiyo na hosteli mojawapo.
 
Dazeni kadhaa za shule zimechomwa moto na idadi isiyofahamika ya wanafunzi wameuawa kati yao zaidi ya waathirika 1,600 wakiuawa na Waislamu wenye msimamo mkali tangu mwaka 2010.
 
Washambulizi hao wamechoma majengo na kufyatulia risasi wanafunzi wakati wakijaribu kujisalimisha, kwa mujibu wa shirika la habari la Reuters. Wanafunzi kadhaa wamekuwa wakitibiwa majeraha ya moto, aliongeza.
 
Yalikuwa matukio matatu mabaya zaidi kuwahi kutokea kwenye shule tangu majeshi yalipoanzisha ulinzi Mei kujaribu kupambana na Boko Haram, kundi la harakati za Waislamu wenye msimamo mkali ambao jina lao linatafsiriwa kama 'Elimu ya Kimagharibi ni haramu' katika lugha ya Hausa eneo la kaskazini.
 
Potiskum ipo katika jimbo la Yobe, moja kati ya tatu zilizowekwa katika hali ya hatari iliyotangazwa na Rais Goodluck Jonathan mwezi Mei, pale alipoamuru vikosi zaidi kwenda kwenye eneo hilo kujaribu kutokomeza kundi hilo linaoonekana kama tishio kubwa zaidi kwa ulinzi wa taifa hilo linaloongoza kwa kuzalisha mafuta barani Afrika.
 
Wanamgambo wanaodhaniwa kuwa wa Kiislamu walimimina risasi kwenye shule moja katika mji ulioko kaskazini mashariki mwa Nigeria wa Maiduguri mwezi uliopita na kuua wanafunzi tisa, na shambulio linalofanana na hilo kwenye shule moja iliyoko katika mji wa Damaturu lililoua wanafunzi saba siku chache tu kabla.
 
Vikosi vya Nigeria vimesema uhalifu wao umewawezesha kurejesha udhibiti wa eneo hilo lisilofikika kwa urahisi la kaskazini mashariki kutoka kwa Boko Haram, wakisambaratisha maeneo muhimu na kukamata wengi wa watuhumiwa.
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

0 comments:

 
Top