Virusi vya HIV hujificha kwenye Uboho (Bone Marrow)
 
Wagonjwa wawili wameondolewa bughdha ya kutumia madawa ya kupunguza makali ya ukimwi maishani mwao baada ya kufanyiwa upasuaji na kupandikiziwa uboho wa binadamu au (Bone marrow), hatua inayosemekana kuondoa virusi vya HIV mwilini mwao.

Mgonjwa mmoja amesemekana kukaa kwa miezi minne bila ya kutumia madawa ya kupunguza makali ya ukimwi bila ya dalili ya kurejea kwa uogonjwa huo.
Matojeo ya utafiti huo yaliwasilishwa katika mkutano wa kimataifa kuhusu maswala ya Ukimwi.

Ni vigumu sana kutibu Ukimwi, kwa sababu hujificha ndani ya DNA, ya mtu na hivyo kusababisha virusi sugu ambavyo haziwezi kutibika.

Madawa ya kupunguza makali ya virusi vya HIV hudhibiti virusi hivyo ndani ya damu lakini wakati mtu anapokosa kumeza dawa hizo, virusi hurejea.

HIV imeangamizwa?
Wanaume hao ambao hawajatajwa majina yao, wameishi na virusi hivyo kwa takriban miaka 30.

Wote walikuwa wanaugua aina ya saratani, aina ya lymphoma, ambayo ilihitaji wafanyiwe upasuaji.

Sehemu ya Uboho au Bone marrow ndipo seli mpya za damu hutengezwa mwilini na inaaminika kuwa kitovu cha virusi vya HIV mwilini.

Baada ya kufanyiwa upasuaji, hapakuwa na virusi mwilini kwa miaka miwili kwa mgonjwa mmoja wakati mwingine aliishi kwa miaka minne bila ya virusi kuonekana.

Ni mapema mno kuona upasuaji huo kama tiba ya ukiwmi na hata ikiwa itasemekana kuwa tiba basi sio tiba nzuri. Ni ghali mno na kwa baadhi ya wagonjwa kuna uwezekano wa kufariki ikiwa kwa asilimia 15 hadi 20% kwa miaka ya kwanza baada ya kufanyiwa upasuaji.

Wagonjwa hao sasa hawatumii tena dawa za kupunguza makali ya ukimwi. Upasuaji huu ulifanyiwa wagonjwa hao kwa sababu waikuwa wanaugua saratani iliyohitaji matibabu.

Mgonjwa mmoja amesemekana kukaa kwa miezi minne bila ya kutumia madawa ya kupunguza makali ya ukimwi bila ya dalili ya kurejea kwa ugonjwa huo.

Hata hivyo, madaktari waliofanya utafiti huo katika hospitali ya matibabu kwa wanawake ya Brigham nchini Marekani, wametahadharisha kuwa ni mapema mno kuzungumzia uwezekano wa kutibu virusi hivyo kwani vinaweza kurejea wakati wowote.

Matokeo ya utafiti huo yaliwasilishwa katika mkutano wa kimataifa kuhusu maswala ya Ukimwi.

Ni vigumu sana kutibu Ukimwi, kwa sababu virusi hujifificha ndani ya DNA, ya mtu na hivyo kusababisha virusi sugu ambavyo haviwezi kutibika.

Madawa ya kupunguza makali ya virusi vya HIV hudhibiti virusi hivyo ndani ya damu lakini wakati mtu anapokosa kumeza dawa hizo, virusi hurejea.
BBCSWAHILI TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

0 comments:

 
Top