sb
Mfalume Mswati III wa Swaziland akitoa hotuba yake wakati wa Uzinduzi Rasmi wa Maonesho ya Biashara ya Kimataifa katika Viwanja vya Sabasaba, Jijini Dares Salaam(Kushoto kwa King Mswati III) ni Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Mizengo Kayanza Pinda.
 sb1
Mfalume Mswati III wa Swaziland(katikati) akiwa amesimama na Meza Kuu wakiimba   Wimbo wa Taifa la Swaziland leo katika Uzinduzi wa Maonesho ya Biashara ya Kimataifa, Jijini Dar es Salaam(wa pili kulia)ni Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Mizengo Kayanza Pinda.
 sb2
Mfalme Mswati III wa Swaziland akiingia katika Viwanja vya Maonesho ya Biashara ya Kimataifa tayari kwa Uzinduzi Rasmi akiwa ameongozana na Mwenyeji wake Waziri Mkuu wa Tanzania, Mhe. Mizengo Pinda.  
 
Picha zote na Lucas Mboje wa Jeshi la Magereza.
 
Mfalme Mswati wa III wa Swaziland amefungua rasmi  maonesho ya kimataifa ya biashara katika viwanja vya mwalimu Nyerere barabara ya Kilwa jijini Dar es Salaam.

Mfalme huyo amepata nafasi ya kutembelea mabanda mbalimbali katika maonesho hayo ya 37 ambayo yalianza Ijumaa ya wiki iliyopita na yanataraji kufikia tamati Julai nane mwaka huu.

Mfalme Mswati III pia alihudhuria mkutano wa kimataifa wa manufaa kwa wote uliofanyika  katika ukumbi wa kimataifa wa  Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam.
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

0 comments:

 
Top