images c94ff
Leo asubuhi Joseph Mbilinyi (Sugu) alipelekwa mahakamani kwa shitaka la kutumia lugha ya matusi dhidi ya Waziri Mkuu, shtaka hili lilifunguliwa kwenye mahakama ya hakimu mkazi wilaya ya Dodoma na mwendesha mashitaka wa serikali.

Baada ya kufunguliwa shtaka hilo, Lissu ambaye alikuwa wakili wa Sugu aliitaka mahakama ifutilie mbali shtaka hilo kwani halina msingi wowote wa kisheria, na baada ya mabishano ya kisheria baina ya Lissu na wanasheria wa serikali kushindwa kuthibitisha kuwa neno Mpumbavu ni lugha ya matusi, hakimu ameamua kufuta shtaka hilo na ametangaza kuwa Sugu yuko huru na hana kesi ya kujibu..

My take:Polisi na serikali, mnaendelea kujidhalilisha kwa kufungua kesi ambazo zinaendelea kuwavunjia heshima, acheni kufuata maelekezo ya kina Mwigulu, hawajui sheria, hawajui misingi ya kufungua kesi, nyie kila siku mtakuwa mnafungua kesi mpaka lini wakati mnashindwa daima mbele ya mahakama na umma wa wa-Tanzania. 
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

0 comments:

 
Top