Jeshi la
Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ)limepokea
taarifa kwamba waandishi wa Habari kadhaa wamepelekwa Mtwara kwenda kumhoji
msichana mmoja kwa madai ya kubakwa na wananjeshi wa JWTZ.
JWTZ
linapenda kuwafahamisha wananchi kuwa endapo taarifa hizo zitatangazwa
kwenye baadhi ya vyombo vya Habari wazipuuze kwani hazina ukweli wowote zaidi
ya kuwa ni za upotoshaji.
Msichana huyo amepandikizwa ili kuharibu taswira
nzuri ya JWTZ. Ifahamike kwamba maafisa na askari wa JWTZ waliopo huko Mtwara
wanafanya kazi kwa uangalizi wa karibu na vitendo hivyo vya aibu hawawezi kuvifanya.
Jeshi letu linafanya kazi kwa
nidhamu na si kama baadhi ya watu wenye maslahi binafsi wanavyolipaka matope.
Tunapenda kuwafahamisha watanzania wote kuwa
JWTZ lipo kwa ajili ya maslahi ya watanzania wote.
Tunasikitika sana kama wapo
watanzania wenye mawazo hayo machafu ya kulichafua
JWTZ lenye sifa nyingi ndani na nje ya nchi yetu.
Imetolewa na Kurugenzi ya Habari na Uhusiano
Makao Makuu ya Jeshi, Upanga
SLP
92023, Simu: 0764 742161
0 comments:
Post a Comment