Asasi ya Vijana  wa  umoja wa  Mataifa Tanzania [ YUNA]  imejipanga kukusanya maoni  kwa vijana nchini ili kuhakikisha wanapata  mawazo ya vijana hao ambayo watayawakilisha katika Umoja wa Mataifa  katika kufikia malengo ya Mellenium.
 
Akizungumza na waandishi wa habari Jijini Dar es Salaam Mwenyekiti wa Taasisi hiyo Bwana LWIDIKO EDWARD   ameelezea jitihada ambazo wamekuwa wakizichukua katika kuhakiki vijana wanahusishwa zaidi katika kufikia malengo ya Milenium  ikiwemo kuzunguka zaidi ya mikoa sita nchi nzima kwa kuwahusisha  wanafunzi wa vyuo na  Sekondari.
 
Mwenyekiti wa Umoja huo ameendelea  kufafanua kuwa  pamoja na Mlengo ya Melinia kuwa na mipango na malengo mengi  lakini  bado vijana wameonekana kuachwa katika malengo hayo hivyo ili kuhakikisha vijana wanaingizwa katika malengo ya melinia yajayo wameandaa mkutano Mjini DODOMA  Katika Jengo la Bunge. 

Kwa upande wa atakatayekuwa  kiongozi wa Mkutano huo CATHERINI FIDELIS,  amesema kuwa nikkwumalayakwanza  vijana wa Tanzania kupata Fursa  ya kuanda  mukutano huo utakaofanyika Tarehe 2 mpaka tarehe 6 ya mwezi ujao.
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

0 comments:

 
Top