Kitengo cha kimataifa cha
upelelezi Nchini Urusi FSB, kinasema kuwa kimewazuilia raia 25 wa
Ukraine, kikiwalaumu kwa kupanga mashambulio ya kigaidi mwezi uliopita
wakati jimbo la Crimea lililokoUkraine lilipokuwa likiandaa kura ya maoni.
Idara hiyo inasema watu hao
wanaozuiliwa walikuwa wanachama wa vuguvugu la ultra-nationalist na
walikuwa wakijiandaa kusababisha mashambulio hayo katikati na kusini mwa
Urusi.
Awali, waziri wa usalama wa taifa wa Ukraine,
Arsen Avakov amesema kuwa tume rasmi ya uchunguzi inaonesha kuwa kitengo
maalum cha polisi kiitwacho Berkut kilichobuniwa kukabiliana na vurumai kiliwauwa waandamanaji kadhaa katika uwanja wa maandamano mjini Kiev, mwezi Februari.
Amasema kikosi hicho maalum cha polisi kimevunjiliwa mbali.
Kaimu Waziri mkuu Arseniy Yatsenyuk ameiambia
BBC kuwa rais aliyengolewa madarakani Viktor Yanukovych na washirika
wake ndio wahusika wakuu katika maafa hayo.
Zaidi ya watu 100 waliuwawa katika vurumai hilo.
Naye kiongozi mkuu wa upelelezi Nchini Ukrainne
Valentyn Nalyvaychenko amesema kuwa idara ya upelelezi ya Urusi imetuma
tani kadhaa za vilipuko na silaha hadi Ukraine.
BBC
0 comments:
Post a Comment