Kamati ya bunge la Marekani kuhusu
ujasusi imeidhinisha kuwekwa wazi kwa sehemu mojawapo ya ripoti
iliyoiita ya "ukatili" iliyoelezea jinsi maofisa wa shiriki la upelelezi
la Marekani (CIA) wanavyowahoji wanaotuhumiwa wa ugaidi.
Lakini wanakamati wanasema kuwa itachukua muda kabla ya uchunguzi huo kuwekwa wazi kwa umma.
Baadhi ya ripoti iliyofichuliwa inasema kuwa
idara ya CIA kila mara ilipotosha serikali kuhusiana na mtindo wake wa
kuhoji washukiwa wa ugaidi wakati wa utawala wa Rais George W Bush.
CIA inapinga baadhi ya matokeo ya taarifa hiyo huku ikikiri kutenda matendo ambayo hayakuafikiana na sera za Marekani.
Mwenyekiti wa kamati hiyo ya bunge la seneti
Dianne Feinstein anasema matokeo ya kura iliyopigwa kuhusu ripoti hiyo
inaonesha wabunge 11-3 waliipigia mswada huo kura huku akiita ni
uchunguzi wa matokeo yanayotamausha.
"ripoti hiyo inaonyesha dhuluma inayoenda kinyume na hadhi ya taifa letu.
Hii inatia doa historia ya taifa letu na ambayo
hairuhusiwi kamwe kufanyika. Hivi sivyo wamarekani wanavyofaa kufanya."
Mwanasiasa huyo wa chama cha Democrat kutoka Carlifonia amesema.
Taarifa ya wanahabari inasema kuwa japo baadhi
ya wanakamati wa chama cha Republican walikashifu ripoti hiyo kwa pamoja
na wa Democrats, kulionyesha waziwazi mgawanyiko uliopo ndani ya
wajumbe hao.
Matokeo ya uchunguzi huo uliyomo katika kijitabu
cha ukurasa 500, yatatumwa kwa Rais Barack Obama ili kuchunguzwa,
kutiwa saini, kisha kutolewa kwa umma.
BBC
0 comments:
Post a Comment