Rais Barak Obama
Rais
Barak Obama wa Marekani, akiambatana na Mke wake Michelle, anatarajiwa kutembelea
nchi za Afrika Kusini, Senegal na Tanzania kuanzia Juni 26 - Julai
3 mwaka huu.
Hii ni kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa jana na Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, Ikulu.
Katika
ziara hiyo Rais Obama anatarajiwa kusisitiza juu ya nafasi ya uhusiano uliopo kati ya Marekani na nchi za Kusini mwa Jangwa la Sahara ambapo ziara hiyo pia italenga
katika kupanua wigo wa kukua kwa uchumi, uwekezaji na biashara; kuimarisha
taasisi za kidemokrasia pamoja na kuwekeza katika kizazi cha viongozi wajao wa
Kiafrika.
Taarifa hiyo imeendelea kusema kuwa Rais
Obama anatarajiwa pia kukutana na viongozi wa serikali, wafanyabiashara,
vikundi vya kiraia, hasa vijana, kwa lengo la kujadili masuala ya mahusiano kati ya nchi na nchi na hata ulimwengu kwa ujumla.
Ziara
hii kwa nchi za Kiafrika inalenga pia katika kusisitiza juu ya mchango wa Rais Obama katika
kupanua na kuimarisha uhusiano kati ya Marekani na watu wa nchi za Kusini mwa
Jangwa la Sahara lengo likiwa kudumisha amani na ustawi wa kikanda na Ulimwengu
kwa ujumla.
Rais Obama ambaye baba yake alizaliwa
Kenya, alizuru Afrika mara moja katika muhula wake wa kwanza,
alipotembelelea Ghana mwaka 2009.
Hii inamaanisha kuwa kwa mara nyingine Rais Obama anashindwa kutembelea Kenya ambayo hata hivyo itafarijika kumwona akitua katika nchi mojawapo katika ukanda wa Afrika Mashariki.
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

0 comments:
Post a Comment